Most searched:

Mimi ni ukumbusho uliosahaulika!

Fursa ya kumtambua Amirul Muuminina (a.s) kupitia kioo cha maneno ya Mwenyezi Mungu; "Aya za Alawi" ni mtazamo wa cheo na hadhi ya Amirul Muuminina (a.s) katika Qur’ani Tukufu.

Aya inayojadiliwa leo ni aya ya 27 ya Surah At-Takwir:

 

Mwenyezi Mungu anasema katika aya ya 27 ya Surah At-Takwir:

 إِنْ هُوَ إِلاَّ ذِكْرٌ لِلْعالَمينَ

« Hii [Qur’ani] si chochote ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote. »

Imamu Baqir (a.s) anasema: « « إِنْ هُوَ إِلَّا ذِکْرٌ لِلْعالَمِینَ »; yaani Amirul Muuminina (a.s). »[1]

Jabir bin Yazid anasimulia:

« Nilimwendea Imamu Baqir (a.s). Akasema: “Kwa hakika Amirul Muuminina (a.s) amesema katika khutba yake: Ukumbusho uliosahaulika na kupotezwa na watu ni mimi; na njia waliyoiacha ni njia yangu.” »[2]

Vyanzo:
[1] Tafsir Ahlulbait (as), juzuu ya 17, ukurasa 418; Al-Kafi, juzuu ya 8, ukurasa 287; Bahr al-‘Irfan, juzuu ya 11, ukurasa 74.
[2] Tafsir Ahlulbait (as), juzuu ya 17, ukurasa 418; Al-Kafi, juzuu ya 8, ukurasa 28; Bahr al-‘Irfan, juzuu ya 11, ukurasa 74.

Yaliyomo zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *