Katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, kila siku tunasikiliza kwa makini neno la thamani kutoka kwa Mkuu wa Ufasaha, Amirul Muuminina (a.s) kuhusiana na mwezi huu uliojaa baraka; ili nuru ya maneno yake matukufu iwe mwongozo kwetu katika kufaidika zaidi na baraka za mwezi huu wa utiifu kwa Mwenyezi Mungu.
Kwa kuanza kwa mwezi wa mapenzi na ibada, mwezi mtukufu wa Ramadhani, hadithi kutoka kwa Amirul Muuminina Ali (a.s) kuhusiana na mwezi huu wa baraka zimekusanywa kwa ajili yenu, wasomaji waheshimiwa, na zitachapishwa kila siku chini ya anwani “Hadithi za Alawi” katika sehemu maalum ya Ramadhani Tukufu.
Hadithi ya siku ya nane
Amirul Muuminina (a.s) anasema:
“Uchamungu kwa Mwenyezi Mungu umewakinga marafiki wa Mwenyezi Mungu na kufanya mambo aliyoyaharamisha, na umeingiza hofu Yake katika nyoyo zao kiasi cha kuwafanya wawe macho nyakati za usiku na kuwafanya wavumilie kiu (kufunga) katika siku za joto; walipendelea taabu kuliko faraja na kiu kuliko kushiba maji, na waliona ajali zao ziko karibu na hivyo wakafanya haraka kutenda mema, wakachukulia matarajio marefu kuwa ni uwongo na hawakusahau mauti.”
اِنّ تقوي الله حَمَت اولياء الله محارمه و ألزمت قلوبُهم مخافَتَهُ حتي اَسْهَرتْ لياليهِم و اجِرَهم فَاُخَذو الراحةَ بالنَّصب وَ الرِّيَّ بِالظَّمَإِ، وَ اسْتَقْرَبُوا الْأَجَلَ، فَبَادَرُوا الْعَمَلَ وَ كَذَّبُوا الْأَمَلَ، فَلَاحَظُوا الْأَجَلَ.
Chanzo
Nahjul Balagha, Khutba ya 114