Katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, kila siku tunasikiliza maneno yenye thamani kutoka kwa Kiongozi wa Fasaha, Amirul Waumini (amani iwe juu yake) kuhusu mwezi huu uliojaa baraka; ili nuru ya maneno yake yenye thamani iwe mwanga wa uongofu kwa ajili yetu kufaidika zaidi na baraka za mwezi huu wa utiifu kwa Mwenyezi Mungu.
Pamoja na kuanza kwa mwezi wa mapenzi na ibada, mwezi mtukufu wa Ramadhani, hadithi kutoka kwa Amiri wa Waumini Ali (amani iwe juu yake) kuhusiana na mwezi huu wa baraka zimekusanywa kwa ajili yenu, wasomaji wapendwa, ambazo zitachapishwa kila siku chini ya unwani “Hadithi za Alawi” katika sehemu maalumu ya Ramadhani Karim.
Hadithi ya Siku ya Pili
Amiri wa waumini (amani iwe juu yake) alisema:
“Katika mwezi wa Ramadhani, zidisheni dua na kuomba msamaha (istighfari); dua inawaondolea mabalaa na shida, na kwa sababu ya kuomba msamaha, dhambi zenu zinafutwa.”
عَلَیکُم فی شَهرِ رَمَضانَ بِکَثرَةِ الُّدُعاءِ و الاسْتِغفارِ: فَأمّا الدُّعاءُ فَیَدفَعُ عَنکُمُ البَلاءَ، و أمّا الاسْتِغفارُ فتُمْحی بِهِ ذُنُوبُکُم.
Chanzo
Fadhail al-Ashhur al-Thalathah, Sheikh Saduq, uk. 108