Amirul Muuminina (amani iwe juu yake) anasema:
“Mtu anayefanya tamaa kuwa nembo yake, amejidhalilisha, na yule anayefichua siri ya shida yake, amekubali unyonge, na yule anayeufanya ulimi wake kuwa mtawala juu ya nafsi yake, amepoteza hadhi na daraja yake.”
Chanzo
Hekima ya pili kutoka Nahjul Balagha