Most searched:

Kutishiwa Vita au Kiapo cha Utii kwa Muawiya

Barua aliyoiandika Amirul Muuminina Ali (amani iwe juu yake) kwenda kwa Jarir bin Abdullah al-Bajali wakati alipomtuma kwa Muawiya (kwa ajili ya kusimamisha hoja ya mwisho).

Matini ya barua hiyo ni kama ifuatavyo:

“Maudhui ya barua hii yako wazi kabisa; Amirul Muuminina Ali (amani iwe juu yake) anataka mjumbe wake Jarir ampe Muawiya hoja ya mwisho kwamba ikiwa yuko tayari kutoa kiapo cha utii, basi atoe kiapo hicho, na ikiwa hayuko tayari, maana yake ni kwamba anakusudia vita.

  • Ama baadaye (baada ya sifa na shukurani kwa Mwenyezi Mungu), barua yangu itakapokufikia, mwalike Muawiya kwenye uamuzi wa mwisho, na ili kukata shauri, mlazimishe kuchukua msimamo thabiti, kisha mpe hiyari kati ya vita vya kuangamiza au kujisalimisha kwenye fedheha. Ikiwa atachagua vita, basi mtangazie vita, na ikiwa atachagua njia ya amani na usalama, basi chukua kiapo cha utii kutoka kwake, Wassalam.”

Chanzo

Barua ya nane kutoka Nahjul Balagha